info@ngomesaccos.co.tz

Fax:  0222 923861

Kuhusu Sisi

Nyumbani Kuhusu Sisi
KUHUSU NGOME SACCOS LIMITED

Historia Fupi ya Chama

NGOME SACCOS LTD ni Chama cha ushirika na akiba na mikopo kilichoanzishwa tarehe 30 Aprili mwaka 2007 kwa mjibu wa sheria namba 20 ya mwaka 2003, Kiliandikiswa katika daftari la Serikali na kupewa usajili DSR 991 kama asasi ya kutoa huduma za kifedha.

Wanachama wake ni "Maafisa, Maaskari, Wastaafu pamoja na watumishi wa Umma wa Wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa na wale waliohamia wizara nyingine wakiwa wanachama Hai wa Ngome SACCOS.

Wasiliana nasi

DIRA

Kuwa SACCOS bora yene kutoa riba nafuu inayoongoza kwenye utoaji wa huduma za kifedha kitaifa na kimataifa

DHIMA

Kukusanya akiba kwa ajili ya kuwakopesha wanachama kwa riba nafuu na kuwaelimisha namna ya kutumia mikopo hiyo kwa busara ya kuwajengea uwezo mkubwa wa kiuchumi na maisha bora.

MISINGI YA CHAMA

Misingi ni suala la muhimu wakati wa kusimamia shughuli za chama kwani husaidia kufikia malengo ya chama kwa wakati. Chama kitazingatia maadili yafuatayo wakati wa kutekeleza shughuli zake:-

1. Ushirikiano/Mshikamano(Solidarity)

Mafanikio ya chama yatafikiwa endapo kutakuwepo na ushirikiano na mshikamo wa karibu kati ya wanachama, Bodi watendaji na wadau wengine. Ni wajibu wa kila mdau kutoa Ushirikiano pale inapohitajika kufanya hivyo.

2. Uwajibikaji (self responsibility)

Viongozi wa chama, Wanachama na watendaji wanapaswa kuwajibika kwa masilahi mapana ya Chama.

3. Kujali wanachama

Mara zote Viongozi wa chama pamoja na watendaji watapaswa kutoa huduma iliyo bora kwa wanachama wake.

4.Uwazi

Shughuli za chama zitaendeshwa katika hali ya uwazi kwa kuzingatia misingi ya kumlinda mwanachama (Consumer protection) pamoja na kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya chama.

5. Ustadi

Bodi pamoja na watendaji watapaswa kuzingatia na kufuata viwango vya kitaalamu walivyonavyo wakati wa kuendesha shughuli za chama.

6.Uaminifu (Honesty)

Viongozi wa chama pamoja na watendaji wanapaswa kuwa waaminifu wakati wa kuendesha shughuli za chama.

7. Kujitolea na kujitegemea (Self help)

Viongozi wa chama na watendaji wanahamasishwa kuwa na moyo wa kujitolea na kujitegemea wakati wote kwa manufaa ya chama na wanachama wake.

8.Uadilifu

Viongozi wanachama na watendaji wanapaswa kuwa waadilifu muda wote.

9. Usawa

Huduma za chama zitatolewakwa misingi ya uwasa.

10. Usiri

Viongozi watatakiwa kutotoa taarifa za chama bila idhini.

Developed by: Ponce Kihaga  


Visit My Portfolio:   poncefolio.com.